Uchaguzi Mkuu wa Kenya, 2007
From Wikipedia, the free encyclopedia
Uchaguzi wa Rais wa mwaka 2007 nchini Kenya ulikuwa na matatizo mengi na kusababisha kipindi cha mvurugo na vifo.
Jamhuri ya Kenya |
Makala hii imepangwa kwa mfululizo: |
|
|
Nchi zingine · Atlasi |
Baada ya Raila Odinga wa ODM kuongoza katika hesabu ya kura kwa muda mrefu Tume ya Uchaguzi ya Kenya lilisimamisha hesabu ya kura kwa muda wa usiku mmoja na baada kuanza upya kura za Mwai Kibaki wa PNU zilikuwa mbele. Tume ikamtangaza Kibaki kuwa mshindi aliyeapishwa mara moja bila kusubiri muda wa kisheria kwa malalamiko. Watazamaji waliona kasoro, makosa na matokeo yaliyodokeza ya kwamba hesabu ya kura ilibadilishwa kwenye ngazi za kupiga jumla za kura kimkoa na kitaifa. Vilevile kuna madokezo ya kwamba kura za kiraisi ziliongezwa katika usiku ambako hesabu ilisimamishwa.
Matokeo yaliyotangazwa ni kama yafuatayo:
- Mwai Kibaki: kura 4,584,721 (asilimia 46.7)
- Raila Odinga: kura 4,352,993 (asilimia 44.3)
- Kalonzo Musyoka: kura 879,903 (asilimia 9)
Wagombea wengine walimaliza kwa kura chache tu.