![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/d0/Santi_Buglioni_-_San_Giovanni_di_Capistrano_c1550.jpg/640px-Santi_Buglioni_-_San_Giovanni_di_Capistrano_c1550.jpg&w=640&q=50)
Yohane wa Kapestrano
From Wikipedia, the free encyclopedia
Yohane wa Kapestrano (Capestrano, wilaya ya L'Aquila, Italia, 24 Juni 1386 - Ilok, katika Korasia ya leo, 23 Oktoba 1456) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki na mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo ambalo alichangia kulirekebisha kufuatana na nia za mwanzilishi, Fransisko wa Asizi.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/d0/Santi_Buglioni_-_San_Giovanni_di_Capistrano_c1550.jpg/640px-Santi_Buglioni_-_San_Giovanni_di_Capistrano_c1550.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/59/Ilok_church.jpg/640px-Ilok_church.jpg)
Alitangazwa kuwa mtakatifu na Papa Aleksanda VIII tarehe 16 Oktoba 1690.
Anaheshimiwa hasa kama msimamizi wa mapadri wanaohudumia wanajeshi.