Angatando

From Wikipedia, the free encyclopedia

Angatando
Remove ads

Angatando (pia angastrato; Kiingereza: stratosphere) ni tabaka mojawapo la angahewa ya Dunia[1]. Inaanza takriban kilomita 8 juu ya uso wa ardhi kwenye eneo la ncha za Dunia lakini juu ya ikweta inaanza kwa kimo cha kilomita 18; inaendelea hadi kimo cha kilomita 50 juu ya uso wa ardhi[2].

Thumb
Matabaka ya angahewa

Katika angastrato, kiunyume na angatropo, halijoto inapanda juu pamoja na kimo. Hii inasababishwa na tabaka la ozoni iliyoko ndani yake. Ozoni hufyonza mnururisho wa urujuanimno kutoka nuru ya Jua na kuibadilisha kuwa joto[3].

Hii ni tofauti na angavurugu iliyoko chini yake. Huko halijoto inapungua kadiri ya kuongezeka kwa kimo. Pia katika angakati iliyoko juu ya tabakastrato halijoto inapungua kadiri ya kufikia juu zaidi.

Hakuna upepo wala mawingu katika angastrato, hivyo eropleni kubwa husafiri pale inapoanza kwenye kimo cha km 12 kwa safari za mbali ambako vurugu kutokana na upepo wa angavurugu zimeshapungua [4].

Remove ads

Marejeo

Viungo vya Nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads