Bahari ya Labrador
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Bahari ya Labrador (kwa Kiingereza: Labrador Sea, kwa Kifaransa: mer du Labrador) ni mkono wa Bahari Atlantiki uliopo baina ya rasi ya Labrador na Greenland. Upande wa kaskazini unaendelea katika Hori ya Baffin kupitia Mlangobahari wa Davis.[1] Imeitwa pia bahari ya pembeni (en:marginal sea ya Atlantiki.[2][3]


Kina cha Bahari ya Labrador kinafikia mita 3400 kwenye kusini inapounganishwa na Atlantiki; katika sehemu hii ina upana wa km 1,000. Upande wa kaskazini kina hupungua hadi mita 700 ikipita kwenye mlangobahari wa Davis.[4]
Halijoto ya maji haipandi juu ya sentigredi 5-6 na wakati wa baridi theluthi mbili za uso wake zinaganda kuwa barafu.
Remove ads
Tanbihi
Viungo vya Nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads