Bahari ya Labrador

From Wikipedia, the free encyclopedia

Bahari ya Labrador
Remove ads

Bahari ya Labrador (kwa Kiingereza: Labrador Sea, kwa Kifaransa: mer du Labrador) ni mkono wa Bahari Atlantiki uliopo baina ya rasi ya Labrador na Greenland. Upande wa kaskazini unaendelea katika Hori ya Baffin kupitia Mlangobahari wa Davis.[1] Imeitwa pia bahari ya pembeni (en:marginal sea ya Atlantiki.[2][3]

Thumb
Ramani ya Bahari ya Labrador
Thumb
Nyangumi na siwa barafu katika Bahari ya Labrador

Kina cha Bahari ya Labrador kinafikia mita 3400 kwenye kusini inapounganishwa na Atlantiki; katika sehemu hii ina upana wa km 1,000. Upande wa kaskazini kina hupungua hadi mita 700 ikipita kwenye mlangobahari wa Davis.[4]

Halijoto ya maji haipandi juu ya sentigredi 5-6 na wakati wa baridi theluthi mbili za uso wake zinaganda kuwa barafu.

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya Nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads