Cheusi Mtungi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Cheusi Mtungi
Remove ads

Cheusi Mtungi ni jina la uhusika kutoka katika tamthiliya ya Siri ya Mtungi kutoka nchini Tanzania. Uhusika umechezwa na Godliver Gordian. Cheusi ni mke wa Cheche Mtungi. Anapitia magumu mengi kwenye ndoa yake lakini anayatatua kwa aina yake. Sifa kuu ya Cheusi ni uvumilivu wake katika ndoa - hasa ukizingatia mumewe ni mtu wa wanawake sana. Sifa nyengine aliyonayo ni pamoja na upole na unyenyekevu kwa mume na mama yake mzazi Bi. Mwanaidi. Hapendi kuyumbishwa kwa ndoa yake na mtu yeyote yule hata kama ni mama yake mzazi ndiye myumbishaji.[1] Kwa upande wa familia aliyozaliwa, yeye ni mtoto wa kwanza wa Bi. Mwanaidi ambaye ni mke wa pili wa Mzee Kizito. Cheusi ni dada wa Shoti, ambaye anaonekana kidogo kuwa na kautahira.

Ukweli wa haraka Imebuniwa na, Imechezwa na ...
Remove ads

Tazama pia

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads