Ukenekaji

From Wikipedia, the free encyclopedia

Ukenekaji
Remove ads

Ukenekaji (kwa Kiingereza: distillation) ni mchakato wa kutenganisha mchanganyiko kiowevu kwa sehemu zake kama sehemu hizi zina viwango vya kuchemka tofauti. Mchakato wa ukenekaji hutumiwa sana katika kemia ingawa si kazi ya kikemia bali ya kifizikia.

Thumb
Ukenekaji katika maabara:
1. Chanzo cha joto (hapa iko jiko la Bunsen)
2. Chupa
3. Kichwa cha ujenekaji
4. Kipimajoto
5. Kitoneshi
6. Maji ya kupoza yanaingia
7. Maji ya kupoza yanatoka
8. Chupa ya kusanya mkeneko

Mchanganyiko hutiwa moto hadi sehemu moja ya mchanganyiko inapochemka yaani inageuka kuwa mvuke. Mvuke huo hukusanywa katika chombo cha kitoneshi (condenser) ambamo unapozwa na kutonesha hadi kuwa kiowevu tena. Kiowevu hicho huitwa mkeneko (distillate).

Mkeneko kwa kawaida bado ni mchanganyiko lakini ina kiwango kikubwa zaidi ya dutu yenye kiwango cha kuchemka cha chini zaidi. Mchakato wote unaweza kurudishwa mara kadhaa ili kuelekea dutu safi zaidi.

Mifano:

Remove ads

Marejeo

Viungo vya Nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads