Mshale (kundinyota)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Kwa habari za sayari (wakati mwingine kwa kosa huitwa pia "Kausi") angalia hapa Neptuni; kwa matumizi mengine ya jina "Sagittarius" angalia hapa Sagittarius


Mshale (pia Kausi, kwa Kilatini/Kiingereza: Sagittarius[1]) ni jina la kundinyota kwenye zodiaki.
Nyota za Mshale huwa haziko pamoja kihalisi lakini zinaonekana tu vile kutoka duniani. Kwa uhalisi kuna umbali mkubwa kati yao, kama ziko mbali au jirani nasi. Kwa hiyo kundinyota "Mshale" linaonyesha eneo la angani jinsi tunavyoiona kutoka Duniani.
Remove ads
Jina
Mabaharia Waswahili wamejua nyota hizi kwa muda mrefu kwa jina la "Kausi" linalotokana na neno la Kiarabu Qaws قوس linalomaanisha "upinde". Maana hii ni karibu sawa na jina la Kilatini "Sagittarius" (mpiga upinde). Wataalamu wa kale waliona katika nyota zake picha ya mtu anayekalia juu ya farasi akishika pinde na kulenga mshale.
Jina la "Kaus" limetumiwa pia katika elimuanga ya kimagharibi kutaja nyota kadhaa zilizomo hapa kama vile Kaus Australis, Kaus Medius na Kaus Borealis.
Katika vitabu kadhaa vya shule za msingi nchini Tanzania "Kausi" imetumiwa kwa kosa kutaja sayari ya nane katika Mfumo wa Jua letu yaani Neptuni.
Katika unajimu wa kisasa jina la Kausi limeshasahauliwa na nyota hizi zinajulikana zaidi kwa “Mshale” ambayo inarejelea picha inayotumiwa kama ishara yake.
Remove ads
Kuonekana
Mshale inaonekana pale angani ambako Njia Nyeupe inang'aa zaidi yaani kuelekea kitovu cha majarra yetu.
Mshale ni kati ya makundinyota yaliyojulikana tangu karne nyingi zikitumiwa hasa na mabaharia kutafuta njia baharini wakati wa usiku.
Nyota na magimba ya anga
Katika eneo la Mshale wataalamu wa anga walitambua magimba ya angani kadhaa ya maana. Hizi ni pamoja na
- Alfa Sagittarii ambayo ni chanzo cha mawimbi ya redio; inaaminiwa ya kwamba mawimbi haya ni dalili za kuwepo kwa shimo jeusi kubwa sana linaloitwa "Sagittarius A*"; linatazamiwa kuwa shimi jeusi kuu kwenye kitovu cha galaksi yetu yaani Njia Nyeupe.
- Nebula kadhaa zilizoandikishwa katika orodha ya Messier kama vile Nebula za Wangwa, Bata-Maji, na Buibui Nyekundu.
Tanbihi
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads