Njia Nyeupe
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Njia Nyeupe (pia "mkokoto wa kondoo za Sumaili" [1]; kwa Kiingereza Milky Way) ni mlia mpana wa nyota nyingi unaoonekana angani wakati wa usiku kama wingu jeupe linalong`aa.



Hali halisi hii ni jinsi tunavyoona galaksi yetu ambamo mfumo wa Jua letu pamoja na Dunia ni sehemu zake.
Remove ads
Umbo na umbali
Galaksi yetu imekadiriwa kuwa na nyota zaidi ya bilioni 100 hadi bilioni 400[2]. Inafanana na kisahani chenye umbo la parafujo. Kipenyo cha kisahani hicho ni miakanuru 100,000 ikiwa na unene wa miakanuru 3,000.
Galaksi iliyo karibu zaidi angani inaitwa Andromeda ikiwa na umbali wa miakanuru milioni 2.5.
Isipokuwa sayari za Jua letu na galaksi ya Andromeda (inayoonekana kama nyota moja), nyota zote ni kama Jua letu yaani tufe kubwa sana la gesi joto.
Remove ads
Kuonekana kwa Njia Nyeupe kutoka duniani
Nyota karibu zote tunazoziona kwa macho yetu ni sehemu za Njia Nyeupe. Kutegemeana na kiwango cha giza tunaweza kuona kati ya nyota 3,000 hadi 6,000 bila msaada wa darubini.
Si rahisi kuona nyota nyingi tukiwa mjini kwa sababu mwanga wa taa za mjini unaakisiwa katika angahewa na kuzuia kuona mianga hafifu nje ya angahewa.
Idadi kubwa zaidi ya nyota za Njia Nyeupe hatuwezi kuona wala kubainisha, kwa hiyo zinatokea machoni kama ukungu mweupe tu.
Uwezo wetu wa kuona nyota nyingi zaidi umepunguzwa na kuwepo kwa mavumbi ya kinyota kati ya mahali petu na kitovu cha galaksi.
Remove ads
Muundo
Galaksi yetu ina umbo la parafujo (spirali) ya kisahani. Mahali petu pamoja na Jua pako kando kiasi ndani ya uwiano wa kisahani hiki. Tuko takriban 2/3 ya umbali wa kipenyo kutoka kitovu cha kisahani.
Ikitazamwa kutoka juu galaksi yetu ina umbo la parafujo yenye mikono mbalimbali. Picha hii tumeipata kutokana na kuangalia galaksi za mbali angani zinazoonekana kutoka juu ilhali parafujo inaonekana.
Soma pia
- Thorsten Dambeck in Sky and Telescope, "Gaia's Mission to the Milky Way", Machi 2008, p. 36–39.
- Cristina Chiappini, The Formation and Evolution of the Milky Way, American Scientist, November/December 2001, pp. 506-515
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads