Kieuskara
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Kieuskara (au Kibaski) ni lugha hai ya pekee[1] inayotumiwa na Wabaski hasa mpakani mwa Hispania kaskazini na Ufaransa kusini-magharibi kwenye milima ya Pirenei karibu na bahari ya Atlantiki.[2]

Ingawa inakubalika ilikuwa inatumika huko kabla ya lugha za Kihindi-Kiulaya kuenea Ulaya magharibi, haieleweki ilianzaje, kwa sababu hakuna lugha yoyote inayofanana nayo.
Wanaoitumia ni kama watu 715,000, wengi wao wakiwa Hispania, ambako inalindwa na kustawishwa zaidi.
Remove ads
Tanbihi
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads