Kusini

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kusini
Remove ads

Kusini ni moja kati ya mielekeo minne mikuu ya dira. Mwelekeo wake ni ncha ya kusini ya dunia. Kinyume chake ni kaskazini.

Thumb
Alama za dira zikionyesha kusini katika hali ya mkoozo

Jina "kusini" laaminiwa limetokana na neno lenye asili ya Misri ya Kale kwa ajili ya nchi ya Kushi iliyokuwepo upande wa kusini wa Misri katika Nubia (au Sudani ya leo) pamoja na Uarabuni ya Kusini. Jina la Kushi lapatikana pia katika masimulizi ya Biblia likimtaja mmoja wa wana wa Hamu katika kitabu cha Mwanzo 10:16 kama baba wa watu wa Kushi. Hili neno lilitumiwa na mabaharia Waarabu pia kutaja mwelekeo wa kusini na kwa umbo la "kusi" hasa upepo wa kusini. [1]

Ukitazama jua linapochomoza kusini huwa ni upande wa kulia. Kusini kawaida huwa chini zaidi kwenye ramani. Marekani ipo kusini mwa nchi ya Kanada, Tanzania ipo kusini mwa nchi ya Kenya, na Msumbiji ipo kusini mwa nchi ya Tanzania. Ncha ya kusini ni kusini ya mbali unayoweza kwenda.

Remove ads

Tazama pia

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads