Margerita wa Youville

From Wikipedia, the free encyclopedia

Margerita wa Youville
Remove ads

Margerita wa Youville (kwa Kifaransa Marie-Marguerite Dufrost de Lajemmerais d'Youville; Varennes, Quebec, 15 Oktoba 1701Montreal, Quebec, 23 Desemba 1771) alikuwa mwanamke Mkristo wa Kanada ambaye, baada ya kufiwa mumewe, alielekeza wanae wawili kwenye upadri akajitosa kwa nguvu zake zote kuhudumia wagonjwa, wazee na wenye shida za kila aina, akaanzisha shirika la kitawa la Masista wa Upendo wa Montreal [1].

Thumb
Marguerite d'Youville alivyochorwa na James Duncan.

Papa Yohane XXIII alimtangaza mwenye heri mwaka 1959, na Papa Yohane Paulo II mtakatifu tarehe 9 Desemba 1990, akiwa wa kwanza mzaliwa wa Kanada[2].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[3] au 16 Oktoba.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads