Mr Nice
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Lucas Mkenda (maarufu kama Mr Nice[1]; alizaliwa Moshi, Tanzania, mwaka 1978) ni mwimbaji mkongwe wa Tanzania na mmoja wa waimbaji mashuhuri waliotawala muziki wa Afrika Mashariki mwanzoni mwa miaka ya 2000.[2]
Alianza kupata umaarufu mwaka 1999 baada ya kutoa albamu yake ya kwanza, Kidali Po, na kuelekea mwisho wa 2002, alitoa albamu yake ya pili, Rafiki, pia nyimbo zake kama; Kikulacho, Fagilia Wote[3] na Kuku Kapanda Baiskeli zilikuwa kati ya nyimbo kuu zilizovuma katika taaluma yake. Alikuwa maarufu kwa mtindo wake wa Takeu staili.
Remove ads
Maisha
Lucas Mkenda kwa sasa anaishi nchini Kenya na mkewe ambaye wana watoto wawili wa kike.
Mnamo 2021, mama wa Mr Nice aliyekuwa akiishi Moshi, Tanzania alifariki dunia.[4]
Diskografia
Albamu
- Kidali po
- Rafiki
Nyimbo
- Kikulacho
- Fagilia
- Nakuita
- Kidalipo
- Awe mama we
- Tabia gani
- Mama
- Tuvumiliane
- Kila mtu na demu wake
- Kuku kapanda baiskeli
- Mbona umeniacha
- King'asti[5]
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads