Murti
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Murti ni neno la Kisanskrit ambalo linamaanisha sanamu ya mungu fulani katika dini ya Uhindu[1]. Kwa imani ya Kihindu murti si mungu mwenyewe bali ishara yake ambamo roho ya mungu inajionyesha[2].

Waumini Wahindu huombea kuwepo kwa mungu katika sanamu ili waweze kuwasiliana naye na kupokea baraka zake. Wahindu hawaziabudu murti au sanamu yenyewe bali mungu ambaye yuko katika roho zao. Murti hupatikana hekaluni lakini ziko pia nyumbani mwa Wahindu wengi kwa matumizi ya ibada.[3]
Remove ads
Nafasi ya murti katika ibada


Murti mara chache hupatikana bila umbo maalumu lakini kwa kawaida ni sanamu za mawe au metali zinazomwonyesha mungu fulani katika umbo la kibinadamu kama vile Shiva au Ganesha, Rama au Krishna, Saraswati au Kali.
Murti huchongwa kulingana na maagizo madhubuti na kisha kuwekwa hekaluni na makuhani wenye mafunzo katika ibada maalumu.
Remove ads
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads