Nebula ya Jabari
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Nebula ya Jabari (ing. Orion nebula, pia Messier 42, M42 na NGC 1976) ni nebula angavu inayoonekana katika kundinyota ya Jabari chini ya nyota tatu za ukanda wake. Mwangaza unaoonekana ni mag 4.0 hivyo inaonekana kama nyota lakini kwa kutumia darubini ndogo inatambuliwa kama doa angavu maana ni nebula..
Chanzo cha nebula hii kilikuwa wingu kubwa la molekuli za hidrojeni lililoanza kujikaza. Mawingu ya aina hii ni sehemu za anga la nje ambako nyota zinazaliwa yaani ambako zinaanza kutokea. Nebula hii inaonekana vema kwa sababu nyota changa ndani yake zinatoa mnururisho wa kuioniza (unaondoa electroni kwenye atomi na kuziacha kwenye hali ya kuwa nachaji hasi au chanya, yaani ioni) unaosababisha kung’aa kwa nebula.
Umbali wa nebula ni takriban miakanuru 1425[2].
Kabla ya karne ya 17 ilijulikana kama nyota ya kawaida. Baada ya kugunduliwa kwa darubini Mfaransa Peiresc alikuwa mtu wa kwanza aliyeiangalia kwenye mwaka 1610 kwa kutumia darubini na kutambua si nyota.[3]
Remove ads
Tanbihi
Viungo vya Nje
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads