Nebula ya Jabari

From Wikipedia, the free encyclopedia

Nebula ya Jabari
Remove ads

Nebula ya Jabari (ing. Orion nebula, pia Messier 42, M42 na NGC 1976) ni nebula angavu inayoonekana katika kundinyota ya Jabari chini ya nyota tatu za ukanda wake. Mwangaza unaoonekana ni mag 4.0 hivyo inaonekana kama nyota lakini kwa kutumia darubini ndogo inatambuliwa kama doa angavu maana ni nebula..

Ukweli wa haraka

Chanzo cha nebula hii kilikuwa wingu kubwa la molekuli za hidrojeni lililoanza kujikaza. Mawingu ya aina hii ni sehemu za anga la nje ambako nyota zinazaliwa yaani ambako zinaanza kutokea. Nebula hii inaonekana vema kwa sababu nyota changa ndani yake zinatoa mnururisho wa kuioniza (unaondoa electroni kwenye atomi na kuziacha kwenye hali ya kuwa nachaji hasi au chanya, yaani ioni) unaosababisha kung’aa kwa nebula.

Umbali wa nebula ni takriban miakanuru 1425[2].

Kabla ya karne ya 17 ilijulikana kama nyota ya kawaida. Baada ya kugunduliwa kwa darubini Mfaransa Peiresc alikuwa mtu wa kwanza aliyeiangalia kwenye mwaka 1610 kwa kutumia darubini na kutambua si nyota.[3]


Remove ads

Tanbihi

Viungo vya Nje

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads