Riyama Ally

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Riyama Ally ni msanii wa maigizo na mwandishi na mtengenezaji wa filamu Tanzania, umaarufu wake ulitokana na kundi la sanaa la Taswira ambalo alicheza kwenye tamthilia ya ' Jabari' iliyokuwa ikionyeshwa na kituo cha luninga cha ITV.[1]

Historia

Riyama Ally ni msanii wa maigizo tangu mwaka 2000 wakati huo akiwa kwenye kundi la sanaa la Taswira, ambayo alicheza kwenye tamthilia ya Jabari kama mtoto aliyegeuzwa kichaa na mama yake ambaye alichanganya dawa alizopewa na mganga ili ampe baba yake.[1]

Mafanikio

Mwaka 2003 alijiunga na kundi la sanaa la Tamba Art Group lililokuwa likizalisha filamu za kiswahili kama ‘Miwani ya Maisha’, ‘Mzee wa Busara’ na nyinginezo nyingi ambapo yeye alicheza kwenye filamu za ‘Nsyuka’ na ‘Fungu la Kukosa’ ambazo pia ni miongoni mwa filamu zilizoandaliwa na kundi hilo.

Licha ya uigizaji wake, Riyama pia ni mtunzi wa hadithi mbali mbali za filamu moja wapo ikiwa ni hiyo yake ya ‘Mwasu’ na nyingine ambayo ameiuzia kampuni ya CB ya Charles Mokiwa, ilioko Uingereza.[1]

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads