Sweet Fanta Diallo

From Wikipedia, the free encyclopedia

Sweet Fanta Diallo
Remove ads

"Sweet Fanta Diallo" ni jina la wimbo ulioimbwa na kutungwa na mwanamuziki wa miondoko ya reggae kutoka nchini Ivory Coast, Alpha Blondy. Wimbo unatoka katika albamu ya Revolution iliyotoka mwaka 1987.[1][2] Ndani ya wimbo, Alpha alikuwa anasumbuliwa na matatizo ya kisaikolojia na kulazwa katika moja ya hospitali huko nchini Ivory Coast. Alipata tiba na kupona kwa asilimia mia moja. Siku moja alifikiria kurudi pale hospitalini kwa minajili ya kutoa shukrani kwa nesi mrembo sana aliyemsimamia hadi kupona aliyetambulika kwa jina la Fanta Diallo. Matokeo yake ya kwenda kutoa shukrani kwa nesi huyo yaliishia butwaani baada ya kuambiwa ya kwamba hakuna nesi mwenye jina hilo katika hospitali ile. Imani yake iliendelea kumwambia ya kwamba yule alikuwa malaika na si mwanadamu kabisa.[3]

Ukweli wa haraka Single ya Alpha Blondy kutoka katika albamu ya Revolution, Imetolewa ...
Remove ads

Orodha ya nyimbo

Kwenye santuri ya wimbo huu kuna nyimbo mbili.

Maelezo zaidi Na., Jina la wimbo ...

Tazama pia

  • Revolution

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads