Mambo Huangamia

riwaya iliyoandikwa na Chinua Achebe From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Mambo Huangamia (kwa Kiingereza "Things Fall Apart") ni riwaya iliyoandikwa na Chinua Achebe.

Kitabu hicho alichokiandika mwishoni mwa miaka ya 1950 kilitolewa mwaka wa 1958 na kumpatia jina kubwa duniani. Hicho, kinaaminika ndicho kitabu chake bora zaidi, ni kitabu kilichosomwa kwa wingi zaidi katika vitabu vya tamthiliya ya Kiafrika.[1]

Hadithi ya riwaya hii imefuatiwa na Hakuna Starehe Tena (1960) na Mshale wa Mungu (1964).

Remove ads

Mkondo wa hadithi

Mhusika mkuu anaitwa Okonkwo, tajiri katika kijiji cha Umuofia. Huyo Okonkwo hufuata vizuri sana mila na desturi za Waigbo ili kumshinda baba yake ambaye ni duni.

Katika kufuata hizo mila alifika hatua ya kumuua mwana wake wa kambo na wanakijiji wakakubali. Siku moja, lakini, Okonkwo kwa bahati mbaya alimuua mwanakijiji mwingine akahukumiwa kuondoka kijijini kwake kwa miaka saba zinavyoamuru mila za kijiji.

Huko uhamishoni Okonkwo alikutana na wamisionari Wazungu, akasikitika sana kugundua mwana wake mwenyewe aliacha mila za Kiigbo na kukubali dini ya Ukristo.

Okonkwo akirudi kijijini baadaye akakuta hata maisha ya kijijini yameathiriwa na hiyo dini mpya. Akaanza kuupiga vita Ukristo, hatimaye lakini aliona kuwa haiwezekani kurudi kwa maisha ya kimila akajiua kwa kujinyonga.

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads