Ziara

From Wikipedia, the free encyclopedia

Ziara
Remove ads

Ziara (kwa Kiingereza: trip au travel) ni nomino inayoashiria kutembea au kuzuru mahala fulani. Inawezekana ukafanya ziara pahala ambapo ni ng'ambo na nchi yako au hata ndani ya nchi yako.

Ziara yaweza kufanywa na mtu mmoja au hata kundi la watu. Ziara hufanywa na familia sanasana wakati wa likizo wakati watoto wako nyumbani na wazazi wamepewa ruhusa ya kupumzika nyumbani.

Thumb
Ziara kwa ndege

Yaweza kufanyika kwa mbinu tofauti za usafiri kama miguu, baiskeli, gari, garimoshi, meli au hata ndege.

Remove ads

Madhumuni ya ziara

Ziara hufanyika kwa sababu tofauti. Waweza ukazuru mahala kwa sababu hizi:

  • Kujifurahisha
  • Kupumzisha akili na mwili
  • Kuona mageni
  • Kujua jamii nyingine na kukagua wanavyofanya mambo
  • Kuchukua wakati kutengeneza uhusiano na watu wengine wa mahala tofauti
Thumb
Usafiri kwa gari moshi

Historia ya ziara

Zamani ziara zilifanywa kwa minajili ya kutafuta riziki au kwa sababu ya usalama iwapo ulipo hapana chakula cha kutosheleza jamii yako au kuna usalama duni. Ziara pia zilifanywa kwa sababu ya biashara za kuchuuza watumwa na bidhaa kama chumvi na mifugo.

Kwa leo hii, ziara hufanywa kwa madhumuni haya lakini watu wamekuwa wakifanya ziara sanasana kwa madhumuni ya raha. Kwa mfano, Wazungu hutembelea Afrika ili waweze kuona wanyamapori na pia kuangalia jamii za Kiafrika. Watu hutembea nchini Israeli ili waweze kusali na kufuata kumbukumbu za Biblia. Watu hutembelea jijini York, Uingereza waweze kuona York Minster na The National Railway Museum. Watu hutembea jijini Las Vegas waweze kucheza kamari na kujitosa katika anasa.

Remove ads

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads