Zumari

From Wikipedia, the free encyclopedia

Zumari
Remove ads
Remove ads

Zumari (kutoka jina la Kiarabu; kwa Kiingereza "flute") ni ala ya muziki inayopigwa kwa kupulizwa mdomoni.

Thumb
Aina mbalimbali za zumari kutoka dunia nzima.
Thumb
Zumari mbalimbali.
Thumb
Zumari za kuungwa.
Thumb
Zumari ya Kihindi ikipigwa kutoka pembeni.

Umbo lake ni kama bomba jembamba upande wa mdomoni na pana upande unaotokea sauti.

Inapatikana kote duniani. Hewa inapulizwa ndani kwa mdomo kupitia shimo; mkondo wa hewa unapita kwenye kona kali ambako unaanza kutingatinga ukisababisha nguzo ya hewa iliyopo ndani ya bomba kutingatinga pia; mitetemo hii ni sauti.

Urefu wa bomba unafanya tabia ya sauti; kama ni fupi linatoa sauti ya juu; kama ni refu lina sauti ya chini.

Zumari nyingi huwa na mashimo kanda yanayofunikwa na kufunguliwa kwa vidole. Kwa kufungua shimo mchezaji anafupisha au kurefusha nguzo ya hewa ndani ya zumari inayotingatinga na kubadilisha sauti hivyo.

Kuna muundo kadhaa:

  • shimo la kupulizia liko upande wa pembeni wa filimbi
  • shimo liko mwanzoni wa bomba la filimbi
  • kuna bomba moja lenye mashimo ya pembeni kwa kubadilisha sauti
  • kuna mabomba bila mashimo ya pembeni yaliyounganishwa pamoja; kila filimbi ina sauti yake na mchezaji anateleza mdomo wake juu ya mashimo ya mabomba akipiga muziki yake.
Remove ads

Tanbihi

Loading content...

Marejeo

Loading content...

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads