Lingua franka
From Wikipedia, the free encyclopedia
Lingua franka [1] (inajulikana pia kama lugha ya daraja, lugha ya kawaida, lugha ya biashara, lugha saidizi, au lugha ya kiungo) ni lugha inayotumiwa ili kufanya mawasiliano yawezekane kati ya makundi ya watu ambao hawashiriki lugha mama au lahaja ya pamoja. Kwa kawaida ni lugha ya tatu ambayo ni tofauti na lugha asili za wazungumzaji.
Jina hilo limechukuliwa kutoka Lingua Franca Mediterania ya zama za kati iliyokuwa lugha ya pijini yenye misingi ya Kilatini iliyotumiwa hasa na wafanyabiashara katika nchi jirani na Bahari ya Mediteranea kuanzia karne ya 11 hadi 19. [2]
Lugha yoyote inayotumiwa mara kwa mara kwa mawasiliano kati ya watu ambao hawashiriki lugha asili inaweza kuitwa lingua franka. [3]
Kwa hiyo pijini ni lingua franka; lugha za krioli zinaweza kutumika pia kwa mawasiliano kati ya vikundi vya lugha. Lakini hata lugha asilia ya taifa fulani linaweza kutumiwa na kuitwa hivi, kama inasomwa na watu wengi wenye lugha tofauti na kutumiwa kwa mawasiliano kati yao. Hivyo mara nyingi lugha ya enzi ya ukoloni imekuwa lugha ya mawasiliano kati ya jamii zenye lugha tofauti ndani ya nchi iliyokuwa koloni zamani.[4]
Kwa mfano, Kiingereza ni lugha asilia nchini Uingereza lakini inatumika kama lingua franka nchini Ufilipino, pamoja na Kitagalog. Vilevile, Kiarabu, Kifaransa, Kimandarini, Kirusi na Kihispania hutumikia madhumuni sawa kama lingua franka za biashara na elimu katika maeneo mbalimbali za Dunia.