Pointe-Noire
From Wikipedia, the free encyclopedia
Pointe-Noire (kwa Kikongo: Ninji) ni mji mkubwa wa pili katika Jamhuri ya Kongo, kufuatia mji mkuu wa Brazzaville. Jiji hili huwa na hadhi ya mkoa tangu mwaka 2004. Kabla ya tarehe hiyo ilikuwa makao makuu wa mkoa wa Kouilou.
Mji ulianzishwa kwenye rasi ndogo katika Bahari ya Atlantiki. Pointe-Noire ni kitovu kikuu cha biashara nchini ikiwa na wakazi 715,334 (2007). [1] Rundiko la mji lina wakazi zaidi ya milioni moja.