Skeli ya ugumu ya Mohs
From Wikipedia, the free encyclopedia
Skeli ya ugumu ya Mohs (skeli ya Mohs) ni skeli ya kupima ugumu wa madini iliyobuniwa na Friedrich Mohs, mtaalamu wa madini kutoka Ujerumani. Mohs alibuni skeli yake inayofafanua ugumu wa madini ikilinganisha jinsi madini ya aina moja yanavyoweza kukwaruza mengine.
Miamba huundwa na madini ya aina moja au zaidi. Kulingana na skeli ya Mohs, ulanga ni laini kabisa: inaweza kukwaruzwa na madini mengine yote. Jasi ni ngumu zaidi: inaweza kukwaruza ulanga lakini si kalsiti (kabonati ya kalisi, calcite), ambayo ni ngumu zaidi. Madini magumu kabisa ni almasi (diamond) ambayo haiwezi kukwaruzwa na kitu kingine chochote.
Skeli ya Mohs inatumia madini kumi kwa kulinganisha ugumu. Hayo ni ulanga, jasi, kalsiti, fluoriti, apatiti, felspa, kwazi, topazi, korundi (mfano rubi), hatimaye almasi.
Skeli ya Mohs iliundwa miaka mingi iliyopita, hivyo si kamili kabisa, lakini wanajiolojia bado wanaitumia kwa sababu ni rahisi kutumika, hasa kwa utafiti nje ya maabara. Ndani ya maabara kuna pia vifaa vinavyoruhusu kupima ugumu halisi.
Ugumu wa Mohs | Madini | Fomula ya kikemia | Ugumu halisi [1] | Picha |
---|---|---|---|---|
1 | Ulanga | Mg 3 Si 4 O 10 (OH) 2 | 1 | |
2 | Jasi | ZABURI 4 · 2H 2 O | 3 | |
3 | Kalsiti | CaCO 3 | 9 | |
4 | Fluoriti | CaF 2 | 21 | |
5 | Apatiti | Ca 5 (PO 4 ) 3 (OH -, Cl -, F - ) | 48 | |
6 | Felspa | KAlSi 3 O 8 | 72 | |
7 | Kwazi | SiO 2 | 100 | |
8 | Topazi | Al 2 SiO 4 (OH -, F - ) 2 | 200 | |
9 | Korundi | Al 2 O 3 | 400 | |
10 | Almasi | C | 1600 |