Aidani wa Lindisfarne
From Wikipedia, the free encyclopedia
Aidani wa Lindisfarne (Ireland, 590 hivi - Northumberland, Uingereza, 31 Agosti 651) ndiye aliyeanzisha kituo cha utawa na kuwa askofu wake wa kwanza kwenye kisiwa cha Lindisfarne.
Kabla hajafika huko alikuwa mtawa katika kwenye kisiwa cha Iona katika nchi ya Uskoti.
Mtu mpole sana, mwenye moyo wa ibada na unyofu katika uongozi, tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana kama mtakatifu kwa kufufua Ukristo katika eneo hilo lote hata akaitwa Mtume wa Northumberland[1].