From Wikipedia, the free encyclopedia
Brazzaville ni mji mkuu wa Jamhuri ya Kongo. Una wakazi 2,308,000 (mwaka 2019) ambao ni sawa na 40% ya wananchi wote.
Jiji la Brazzaville | |
Nchi | Jamhuri ya Kongo |
---|
Uko kando ya mto Kongo ukitazamana na mji wa Kinshasa ng'ambo ya mto.
Brazzaville una bandari kwenye mto Kongo na mwanzo wa reli kuelekea pwani.
Jina la Brazzaville limetokana na Mfaransa Pierre Savorgnan de Brazza aliyenunua hapa ardhi kutoka kwa chifu Makoko na kujenga kituo kilichokua na kuwa mji baadaye.
Tangu mwaka 1898 Brazzaville ulikuwa mji mkuu wa Kongo ya Kifaransa ukawa na wakazi 5,000 mnamo 1900 walioongezeka kuwa lakhi moja mwaka 1950.
Mwaka 1940 Brazzaville ulikuwa kwa muda mfupi mji mkuu wa Ufaransa Huru yaani Ufaransa usio chini ya Ujerumani hadi kuhamia kwa serikali hiyo kwenda Algiers.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.