From Wikipedia, the free encyclopedia
Chiapas (jina rasmi: Estado Libre y Soberano de Chiapas; Kiswahili: dola huru la kujitawala la Chiapas) ni moja kati ya majimbo 31 ya Mexiko. Ni jimbo kwenye ncha ya kusini ya
nchi. Mji mkuu na mji mkubwa ni Tuxtla Gutiérrez.
Imepakana na Oaxaca, Tabasco, Veracruz na nchi ya Guatemala. Kunako mwaka wa 2005, idadi ya wakazi ilikuwa 4,293,459. Eneo la jimbo ni 74,211 km².
Kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi. Mazao ya soko ni kahawa, asali na miwa. Kwa jumla eneo halikuendelea sana na wakazi ni kati ya watu maskini zaidi wa Meksiko.
Gavana wa jimbo ni Juan José Sabines Guerrero.
Lugha ni Kihispania na Kimaya.
Makala hii kuhusu maeneo ya Mexiko bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Chiapas kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.