Darubini ya redio
From Wikipedia, the free encyclopedia
Darubini ya redio ni antena maalum na kipokeaji cha redio kinachotumiwa kutambua mawimbi ya redio kutoka kwa vyanzo vya redio kwenye anga-nje. [1] [2] [3] Darubini za redio ndizo vyombo vikuu vya uchunguzi vinavyotumika katika astronomia redio, ambayo huchunguza mawimbi ya redio yanayotolewa na violwa vya anga-nje kama vile nyota, galaksi au nebula. Hivyo zinalingana na darubini nuru zinazochungulia mawimbi ya nuru yanaotoka kwenye violwa vya anga-nje. Tofauti na darubini za nuru, darubini za redio zinaweza kutumika wakati wa mchana na usiku[4].