Hotuba ya mlimani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Hotuba ya mlimani (Math 5:1-7:28) ni hotuba maarufu ya Yesu kwa umati mkubwa uliomkusanyikia katika mlima fulani wa Galilaya. Inatunza maadili maalumu ya Ukristo kulingana na yale ya Uyahudi, hasa ya Mafarisayo na walimu wa sheria ya Musa.
Maelezo zaidi Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu, Mazingira ya Yesu ...
Funga
Kiini chake kinafanana na Hotuba ya mahali tambarare katika Injili ya Luka (6,17-49).
Hotuba hiyo ilizingatiwa sana na Mahatma Gandhi na Martin Luther King katika kupigania haki za binadamu bila ya kutumia mabavu.