Jibuti
From Wikipedia, the free encyclopedia
Jibuti (Kifaransa: Djibouti; Kiarabu: جيبوتي), kirasmi Jamhuri ya Jibuti, ni nchi ndogo ya Afrika ya Mashariki kwenye Pembe la Afrika.
Ukweli wa haraka Jamhuri ya Jibuti, Mji mkuu na mkubwa nchini ...
Jamhuri ya Jibuti | |
---|---|
جمهورية جيبوتي (Kiarabu) République de Djibouti (Kifaransa) Jamhuuriyadda Jabuuti (Kisomali) Gabuutih Ummuuno (Kiafar) | |
Kaulimbiu ya taifa: اتحاد، مساواة، سلام (Kiarabu) Unité, Égalité, Paix (Kifaransa) Midnimo, Sinnaan, Nabad (Kisomali) Inkittiino, Qeedala, Wagari (Kiafar) "Umoja, Usawa, Amani" | |
Wimbo wa taifa: Jibuti | |
Mahali pa Jibuti | |
Ramani ya Jibuti | |
Mji mkuu na mkubwa nchini | Jibuti 11°36′ N 43°10′ E |
Lugha rasmi | |
Lugha za taifa | |
Makabila (asilimia) | 60 Wasomali 35 Waafar 5 Waarabu |
Serikali | Jamhuri yenye mdikteta |
• Rais | Ismaïl Omar Guelleh |
Eneo | |
• Eneo la jumla | km2 23 200[1] |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2023 | 976 143[1] |
Pato la taifa | Kadirio la 2023 |
• Jumla | USD bilioni 3.873[2] |
• Kwa kila mtu | USD 3 761[2] |
Pato halisi la taifa | Kadirio la 2023 |
• Jumla | USD bilioni 7.193[2] |
• Kwa kila mtu | USD 6 985[2] |
Sarafu | Faranga ya Jibuti |
Majira ya saa | UTC+3 (Afrika Mashariki) |
Upande wa magari | Kulia |
Msimbo wa simu | +253 |
Msimbo wa ISO 3166 | DJ |
Jina la kikoa | .dj |
Funga
Imepakana na Eritrea, Ethiopia na Somalia upande wa bara. Kuna pwani ya Bahari ya Shamu na Ghuba ya Aden. Ng'ambo ya bahari iko nchi ya Yemen katika umbali wa km 20 pekee.