Kurudi Nazareti
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kurudi Nazareti kwa familia takatifu kutoka Misri ni tukio la utotoni mwa Yesu linalosimuliwa na Injili.
Maelezo zaidi Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu, Mazingira ya Yesu ...
Funga
Mathayo na Luka sawia wanashuhudia kuwa Yesu alizaliwa Bethlehemu akakulia Nazareti[1][2].
Jambo linalosimuliwa na Injili ya Mathayo tu ni kwamba katikati Yosefu alielekezwa na malaika kukimbilia Misri na Bikira Maria na mtoto Yesu ili kukwepa maangamizi yaliyopangwa na Herode Mkuu dhidi ya watoto wachanga wa kiume wa Bethlehemu. Baada ya Herode kufariki[3][4][5], Yosefu alielekezwa tena kwenda kuishi Galilaya, si Yudea alipotawala Arkelao.[6][7]
Upande wake Injili ya Luka inasimulia tu kuwa Yosefu alikuwa anaishi Nazareth kabla ya Yesu kuzaliwa akarudi huko baada ya Yesu kutolewa hekaluni siku ya arubaini baada ya kuzaliwa.