Mialekundu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mialekundu[1] (pia: infraredi, inforedi) ni aina ya nuru isiyoonekana kwa macho ya kibinadamu lakini kuna wanyama wanaoweza kuiona. Inasikika kama joto. Kifizikia ni aina ya mnururisho sumakuumeme mwenye mawimbi marefu kuliko nuru ambayo inaonekana kwa binadamu na mawimbi ambayo ni mafupi kuliko mawimbi mikro.