![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/51/Bundesarchiv_Bild_146-2005-0151%252C_%25C3%259Cbergang_Helgolands_an_das_Deutsche_Reich.jpg/640px-Bundesarchiv_Bild_146-2005-0151%252C_%25C3%259Cbergang_Helgolands_an_das_Deutsche_Reich.jpg&w=640&q=50)
Mkataba wa Helgoland-Zanzibar
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mapatano baina Uingereza na Ujerumani kuhusu Afrika na Helgoland (kifupi mkataba wa Helgoland-Zanzibar) yalifanywa kati ya Ujerumani na Uingereza tarehe 1 Julai 1890. Pande zote mbili zilielewana juu ya mipaka ya makoloni yao au maeneo walimotaka kuwa na athira kuu katika Afrika.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/51/Bundesarchiv_Bild_146-2005-0151%2C_%C3%9Cbergang_Helgolands_an_das_Deutsche_Reich.jpg/640px-Bundesarchiv_Bild_146-2005-0151%2C_%C3%9Cbergang_Helgolands_an_das_Deutsche_Reich.jpg)
Ukweli wa haraka Uendo, Ukoloni ...
Funga
Mkataba ulihusu maeneo katika Afrika ya Mashariki, Afrika ya Kusini-Magharibi (leo Namibia) na Afrika ya Magharibi (Togo ya leo) pamoja na kisiwa cha Helgoland mbele ya pwani ya Ujerumani katika Bahari ya Kaskazini.