Monsuni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Monsuni ni upepo wa majira unaoendelea kwa muda wa miezi kadhaa kuelekea upande mmoja na kubadilika baada ya kipindi hiki kuelekea kinyume.
Neno hili lilitumiwa mara ya kwanza katika eneo la Bahari Hindi [1] ambako inajirudiarudia kwa nguvu hasa.
Mabaharia Waswahili huwa na maneno tofauti, kutegemeana na mwelekeo wa upepo huo kimajira: musimi au kaskazi, na kusi au demani[2].
Monsuni inapeleka hewa yenye unyevu mwingi kutoka baharini hivyo kuwa na mvua nzito.
Sasa neno latumiwa pia kwa pepo zinazofuata utaratibu wa kufanana katika sehemu nyingine za dunia kama vile Asia ya Kusini-Mashariki au Amerika Kusini.