Mzumai (Chrysopogon zizanioides) au mkasikasi ni spishi ya nyasi katika nusufamilia Andropogoneae. Kwa asili spishi hii inatoka Uhindi lakini siku hizi hupandwa sana katika ukanda wa tropiki. Nchi kuu za uzalishaji ni Haiti, Uhindi, Java na Reunion.
Mzumai | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Mizumai ikitoa mbegu (Chrysopogon zizanioides) | ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
|
Mzumai hupandwa sana kwa kuzuia mmomonyoko kwa sababu mizizi yake inapenya ardhi hadi m 3-4. Majani yanaweza kutumika kwa kulisha wanyama na kwa kutengeneza kamba, mikeka, vikapu n.k.. Mafuta yanasindikwa kutoka mizizi ambayo hutumika katika utamaradi, sabuni ya kiayurveda, dawa za ngozi na tendwa ya harufu.
Picha
- Mizizi ya mzumai sokoni kwa Reunion
- Mafuta ya mzumai
- Kipepeo kilichotengenezwa kwa vitembwe vya mzumai
Wikiwand in your browser!
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.