Papias
From Wikipedia, the free encyclopedia
Papias (70 hivi - 155 hivi) alikuwa mfuasi wa Mtume Yohane pamoja na Polikarpo.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/63/Papias.png/220px-Papias.png)
Baadaye akawa askofu au kiongozi wa ushirika wa Kikristo mjini Hierapoli (karibu na Pamukkale ya leo katika Uturuki).
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 22 Februari[1].