Punt
From Wikipedia, the free encyclopedia
kwa eneo la kujitawala katika kaskazini ya Somalia angalia Puntland
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/7/75/Queen_of_punt.jpg)
Punt (iliitwa pia Pwenet au Pwene[1] na Wamisri wa Kale) ilikuwa milki katika Zama za Kale. Habari zake zinajulikana kutokana na taarifa za Wamisri wa Kale waliofanya biashara nayo. Ilikuwa na sifa za kuzalisha dhahabu, ubao wa mpingo, meno ya ndovu na uvumba zilizotafutwa sana nchini Misri. [2]