From Wikipedia, the free encyclopedia
Wastigmatini (kutoka jina la Shirika la Madonda Matakatifu, ambayo kwa Kilatini yanaitwa Stigmata) ni shirika la kitawa la kikleri la Kanisa Katoliki. Jina rasmi ni Congregatio a Sacris Stigmatibus Domini Nostri Iesus Christi, kifupisho chake ni C.S.S.
Wastigmatini walianzishwa na mtakatifu Gaspare Bertoni tarehe 4 Novemba 1816 huko Verona, Italia.
Katiba ya kwanza ilifuata kielelezo cha ile ya Wajesuiti iliyoandikwa na Ignas wa Loyola.
Shirika lilikua polepole: mwaka 1905 liliingia Marekani na mwaka 1910 Brazil.
Halafu China, Uthai, Ufilipino na nchi mbalimbali za Afrika (zikiwemo Afrika Kusini, Botswana, Ivory Coast, Tanzania) na Amerika (Kanada na Chile).
Mwaka 2012 walikuwa 422, wakiwemo mapadri 331, katika nyumba 92.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.