![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/00/Mary_Salome_and_Zebedee_with_their_Sons_James_the_Greater_and_John_the_Evangelist.jpg/640px-Mary_Salome_and_Zebedee_with_their_Sons_James_the_Greater_and_John_the_Evangelist.jpg&w=640&q=50)
Zebedayo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Zebedayo (kwa Kigiriki Ζεβεδαῖος, Zebedaios, kutoka Kiebrania זְבַדְיָה, Zvad'yah[1], yaani Mwingi au Zawadi yangu[2]), kadiri ya Injili zote nne, alikuwa baba wa Mitume wawili wa Yesu Kristo: Yakobo Mkubwa na Yohane.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/00/Mary_Salome_and_Zebedee_with_their_Sons_James_the_Greater_and_John_the_Evangelist.jpg/320px-Mary_Salome_and_Zebedee_with_their_Sons_James_the_Greater_and_John_the_Evangelist.jpg)
Injili zinamtaja pia mke wake, Salome[3], ambaye pia alifuatana na Yesu hadi kifo chake msalabani huko Kalivari, nje kidogo ya ngome ya Yerusalemu.
Zebedayo aliishi kwenye Ziwa Galilaya[4] na kuwa mvuvi mwenye wafanyakazi chini yake (Mk 1:19-20; Math 4:21-22; Lk 5:4)[4][5]
Injili zinamtaja pia katika mistari mingine: Math 10:2; 20:20; 26:37; 27:56; Mk 3:17; 10:35; Lk 5:10 na Yoh 21:2.