Akademia

From Wikipedia, the free encyclopedia

Akademia
Remove ads

Akademia (kutoka neno la Kigiriki Ἀκαδήμεια, ambalo baadaye likawa Ἀκαδημία akademia) ni shule au chuo kinachotoa elimu au taaluma maalumu, k.v. lugha, muziki, michezo au sanaa.

Thumb
Akademia ya Athens, jinsi alivyoiwaza mchoraji Raffael miaka 2000 baadaye


Jina linarejelea taasisi iliyoundwa na Plato kwenye mwaka 385 KK ilikuwa chuo chake cha falsafa mjini Athens iliyokuwepo ndani ya hekalu ya Athena, mungu wa hekima na elimu.

Pia inaweza kuwa kundi la wasomi wenye ujuzi mkubwa katika taaluma fulani, k.v. siasa, uchumi au masuala ya jamii.

Tena inaweza kuwa taasisi rasmi inayohamasisha maendeleo ya fasihi, sayansi n.k.

Nchi nyingi huwa na "Akademia ya Sayansi" ambayo ni shirika za wataalamu au pia taasisi za wataalamu. Zinalenga kujenga na kuimarisha ushirikiano wa wataalamu wa fani mbalimbali, mbali na kazi yao kwenye vyuo vikuu[1]. Akademia ya Sayansi hailengi kufundisha, inalenga kuunganisha wataalamu na tafiti zao.

Remove ads

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads