Baalbek
mji ulio Lebanon From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Baalbek (/ ˈbɑːlbɛk, ˈbeɪəlbɛk /; kwa Kiarabu: بعلبك, romanized: Baʿlabakk, Syriac-Aramaic: ܒܥܠܒܟ) ni mji uliopo mashariki mwa Mto Litani katika Bonde la Beqaa la Lebanoni takribani kilomita 67 (maili 42) kaskazini mashariki mwa Beirut[1], ni mji mkuu wa mkoa wa Baalbek-Hermel.[2] Katika nyakati za Kigiriki na Kirumi Baalbek pia alijulikana kama Heliopolis (Ἡλιούπολις, Kigiriki kwa "Sun City"). Mnamo mwaka 1998 Baalbek ilikuwa na idadi ya watu 82,608, wengi wao wakiwa Waislamu wa Shia, ikifuatiwa na Waislamu wa Sunni na Wakristo.[3]

Ndipo linapopatikana hekalu la Baalbek ambalo linajumuisha magofu mawili makubwa na makuu ya Kirumi, nayo ni Hekalu la Bacchus na Hekalu la Jupita. Mnamo mwaka 1984 iliandikwa katika orodha ya Urithi wa Dunia ya UNESCO.
Remove ads
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads