Basili Mzee

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Basili Mzee (alifariki Kaisarea ya Kapadokia karne ya 4) alikuwa mtoto wa Makrina Mzee, halafu mhubiri maarufu huko Caesarea Mazaca[1]. Yeye na mke wake Emelia wa Kaisarea walijulikana kwa imani yao[2] iliyowafanya wafukuziwe jangwani wakati wa dhuluma ya kaisari Maximian[3].

Familia yao ilikuwa na watoto 10, waliosaidiwa malezi na bibi yao, Makrina Mzee. Babu yao alikuwa mfiadini. Wote wawili wanaheshimiwa kama watakatifu, kama vile Basili Mkuu na watoto wao wengine 4: Makrina Kijana aliyekuwa mmonaki, Petro wa Sebaste aliyekuwa askofu na mwanateolojia huko Armenia, Naukratio aliyekuwa mkaapweke, na Gregori wa Nisa ambaye alifanywa na Basili kuwa askofu wa Nisa|mji huo akaandika vitabu bora kuhusu teolojia na maisha ya Kiroho[4][5].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[6].

Sikukuu yake huadhimishwa hasa tarehe 30 Mei pamoja na mke wake [7].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads