Benedictus
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Benedictus ni neno la Kilatini lenye maana ya "Asifiwe". Ni maarufu kama jina la wimbo wa Kiinjili unaotumika kila siku katika Masifu ya asubuhi ya madhehebu mbalimbali ya Ukristo.

Jina hilo linatokana na kwamba ndilo neno la kwanza katika tafsiri ya Kilatini ya wimbo huo ambao, kadiri ya Lk 1:68-79, Zakaria aliutunga siku ya kumtahiri ya mtoto wake, Yohane Mbatizaji. Katika nafasi hiyo alifungua tena kinywa chake na kutoa unabii.
Kabla ya hapo, kwa zaidi ya miezi tisa Zakaria alikuwa bubu na kiziwi kama adhabu ya kutosadiki mara maneno ya Malaika Gabrieli aliyetumwa na Mungu kumpasha habari ya kwamba sala zake na za mke wake Elisabeti zimekubalika, hivyo watazaa mtoto wa kiume, ingawa wote wawili ni wakongwe na Elisabeti ni tasa.
Remove ads
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads