David Hilbert
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
David Hilbert (1862 - 1943) alikuwa mtaalamu wa hisabati, mantiki na falsafa ya hisabati kutoka nchini Ujerumani. Huhesabiwa kati ya wanahisabati muhimu zaidi ya karne ya 19 na mwanzo wa karne ya 20.

Alishughulika maswali ya "invariant theory" na ukubalifu wa jiometria. Aliunda hisabati ya nafasi ya mawanda (dimension) nyingi yaani zaidi ya mawanda 2 ya bapa au mawanda 3 ya nafasi ya kawaida. Hilbert na wanafunzi wake waliandaa sehemu kubwa ya hisabati ilyohitajika kwa ajili ya nadharia ya uhusianifu iliyokamilishwa baadaye na Albert Einstein.
Hilbert alizaliwa tar. 23 Januari 1862 mjini Königsberg katika jimbo la Prussia ya Mashariki [1] Alisoma hisabati kwenye chuo Kikuu cha Königsberg, akachukua digrii ya dokta akaendelea kuwa profesa wa hisabati kwanza Königsberg, halafu Göttingen alipokufa tar. 14 Februari 1943.
Remove ads
Viungo vya Nje
- Hilbert's 23 Problems Address
- Hilbert's Program
- Works by David Hilbert katika Project Gutenberg
- Hilberts radio speech recorded in Königsberg 1930 (in German) Ilihifadhiwa 14 Februari 2006 kwenye Wayback Machine., with English translation Ilihifadhiwa 12 Novemba 2020 kwenye Wayback Machine.
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads