Dini za Abrahamu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Dini za Abrahamu
Remove ads

Dini za Abrahamu, ni dini zenye asili katika Mashariki ya Kati ambazo zinashika imani katika Mungu mmoja tu.[1]

Thumb
Nembo za dini za Abrahamu: juu kushoto msalaba wa Ukristo, nyota na hilali vya Uislamu, nyota ya ncha tisa ya Bahá'í, nyota ya Daudi ya Uyahudi.
Thumb
Dini kuu duniani na asilimia ya waumini kati ya binadamu wote.

Asili

Dini hizo zinamchukua Abrahamu kama kielelezo cha mwamini na rafiki wa Mwenyezi Mungu.[2][3] Dini kuu za jamii hiyo (kadiri ya tarehe ya kutokea) ni: Uyahudi (KK), Ukristo (karne ya 1 BK) na Uislamu (karne ya 7),[4][5][6][7] mbali na nyingine ndogo zaidi zilizotokana nazo, kama Baha'i (karne ya 19).

Uenezi

Inakadiriwa kwamba 54% za watu wote duniani wanafuata mojawapo kati ya dini hizo, zikiwemo: Ukristo (33%), Uislamu (21%) na Uyahudi (0.2%).[8][9]

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads