Eris

From Wikipedia, the free encyclopedia

Eris
Remove ads

Erisi (alama: ⯰;[1] pia (136199) Erisi au 136199 Erisi) ni sayari kibete kubwa inayojulikana katika mfumo wa Jua letu.

Thumb
Picha inaonyesha mwendo wa Erisi kwenye picha zilizopigwa kwa darubini ya anga ya Mt. Palomar. Erisi ni ile nukta ndogo inayochezacheza upande wa kushoto juu ya mstari wa katikati ya picha. Mwendo unaoonekana ni mabadiliko ya mahali pa Eris angani katika muda wa masaa matatu. Nukta nyingine ni nyota tu zinazokaa mahali pamoja.
Thumb
Picha ya Erisi na mwezi wake
Remove ads

Tabia ze Erisi

Njia yake ya kuzunguka jua ni nje ya njia ya Pluto. Eros inaonekana ina angalau mwezi mmoja unaoitwa Dysnomia. Makadirio ya kipenyo chake ni 2400 km ambacho ni kikubwa kidogo kuliko Pluto. Inazunguka jua katika muda wa miaka 556.7 ya dunia. Umbali wake na jua ni mara 97 umbali wa dunia yetu. Kutoka Erisi hata jua letu laonekana kama nyota ndogo tu.

Kutambuliwa kwa Erisi

Erisi ilitambuliwa 2005 na wanaastronomia walioongozwa na Dr. Michael E. Brown kwenye paoneaanga Mount Palomar (Marekani). Walichungulia picha za anga zilizopigwa mwaka 2003 wakatambua nukta ya anga lililobadilika mahali.

Erisi ni chanzo cha utaratibu wa "Sayari Kibete"

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads