Ermengol wa Urgell

From Wikipedia, the free encyclopedia

Ermengol wa Urgell
Remove ads

Ermengol wa Urgell (pia: Armengol au Armengod au Hermengaudius; alifariki El Pont de Bar, 1035) alikuwa askofu wa Urgell kuanzia mwaka 1010.

Thumb
Mt. Ermengol katika mavazi ya askofu.
Thumb
Masalia ya Mt. Ermengol.
Thumb
Wasia wa Mt. Ermengol, Arxiu Comarcal de l'Alt Urgell.

Mtoto wa ukoo tawala[1][2], alianza uaskofu wake kwa kurekebisha maisha ya mapadri wa kanisa kuu kufuatana na mafundisho ya Agostino wa Hippo

Anatajwa kama mhusika wa kuteka mji wa Guissona mwaka 1024 na kuurudisha kwenye Ukristo.

Alishindana mara nyingi na masharifu wa Urgell na kuwajibika katika ujenzi wa miundombinu, likiwemo kanisa kuu la Urgell. Akiwa anafanya kazi kwa mikono yake kujenga daraja, alianguka chini akavunjika kichwa kwenye mawe [3].

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3 Novemba[4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads