Kitabu cha Ezekieli
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Kitabu cha Ezekieli kinamhusu mmojawapo kati ya manabii muhimu zaidi wa Agano la Kale, Ezekieli, aliyefanya kazi ya unabii miaka 592-570 hivi K.K., kadiri ya ushahidi wa kitabu chake.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.
Mazingira
Baada ya maangamizi ya Yerusalemu, polepole Wayahudi waliohamishiwa Babeli waliweza kujitafutia kazi (kwanza kilimo, halafu biashara), wakafaulu sana, hata wengine wakawa watumishi wa serikali.
Lakini upande wa dini walikuwa hatarini, kwa sababu imani ya Mwisraeli inategemea taifa, nchi na hekalu ambavyo vyote vilikuwa vimeharibika.
Kwa ajili yao Mungu akatuma tena manabii, hasa Ezekieli ambaye anaonekana kuwa alihamishwa mapema tangu mwaka 598 K.K. pamoja na viongozi wengine 8,000 hivi.
Habari zake tunazipata katika kitabu chake tu, anapotajwa kwa jina mara tatu, kumbe kwa kawaida Mungu anamuita “binadamu”. Kabla hajahamishwa aliweza kumfahamu nabii Yeremia, na kweli aliathiriwa na ujumbe wake ambao aliuunga mkono na kuuendeleza.
Remove ads
Kazi ya Ezekieli
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads