Goregore

Ndege wa jenasi Phoeniculus, familia Phoeniculidae From Wikipedia, the free encyclopedia

Goregore
Remove ads

Goregore (pia golegole), gegemela au vinuka ni ndege wa jenasi Phoeniculus katika familia Phoeniculidae. Hawa ni ndege weusi wenye mkia mrefu na domo refu jekundu au jeusi lililopindika. Mwangani kwa jua manyoya yao yana mng'ao kijani au zambarau wa metali. Kuna mabaka meupe kwa mabawa na mkia. Hupenda kuwa kwa makundi na hupiga kelele pamoja mara kwa mara wakitetea. Inaelekea kama sauti yao ni asili ya jina “gegemela”. Hula wadudu ambao wanawatafuta katika nyufa za miti kama vigong'ota. Jike huyataga mayai 2-4 ndani ya tundu la kiasilia la mti au tundu la zuwakulu au kigong'ota. Baina ya kundi la kama ndege kumi ipo jozi moja tu inayozaa. Ndege wengine wasaidia hawa wawili kutunza makinda.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Remove ads

Spishi

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads