Historia ya China
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Historia ya China inahusu eneo ambalo leo linaunda Jamhuri ya Watu wa China lakini hasa maeneo yote yanayopakanwa na Nyanda za Juu za Tibet upande wa magharibi, Jangwa la Gobi upande wa kaskazini, Myanmar (Burma), Laos na Vietnam upande wa kusini- magharibi na bahari upande wa mashariki. [1]

Vyanzo
Jamii za kwanza zilizoendelea kuwa sehemu za utamaduni wa Kichina zilikalia bonde la Mto Huang He (Mto Njano). Kutoka hapa zilienea polepole zikiathiri makabila mengine. Wakati wa Nasaba ya Han (206 KK – 220 KK) , maeneo mengi ya china ya kihistoria yaliathiriwa tayari na utaaduni ulioanzishwa kwenye kaskazini. Kote hapa ilienea polepole lugha ya kimaandishi ya pamoja, imani kwa nguvu ya mbingu na mizimu na mtazamo wa pamoja kuhusu umuhmu wa matendo na sadaka maalumu zinazolenga kujenga upatanifu mzuri baina ya mbingu, mazingira asilia na binadamu.
Historia ya China hugawanyika katika vipindi vya nasaba za kifalme mbalimbali. Vipindi muhimu zaidi ni kama ifuatavyo:
Remove ads
Nasaba kabla ya maungano ya China
Kabla ya kuunganiswa kwa China kulikuwa na madola mbalimbali. Kati ya madola hayo kuna hasa nasaba tatu zilizoacha ushahidi wa kihistoria:
- Nasaba ya Xia (2200 KK – 1600 KK)
- Nasaba ya Shang (1570 KK – 1066 KK)
- Nasaba ya Zhou (1046 KK – 256 KK)
- Enzi ya milki zilizoshindana (475 KK - 221 KK)
Katika kipindi hicho yalitokea mabadiliko kutoka teknolojia ya mawe hadi bronzi na baadaye chuma. Misingi ya falsafa na dini ya Utao na pia Ukonfusio iliwekwa wakati wa Zhou.
Remove ads
Nasaba tangu kuunganishwa kwa China
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads