Jennifer J. Kayombo

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Jennifer J. Kayombo ni binti mwenye umri wa miaka 21, alisoma chuo kikuu akichukua masomo ya stashahada ya mipango ya miradi, usimamizi na maendeleo ya jamii. Pia ni kiongozi wa vijana, mwanaharakati wa mambo ya wanawake, kwa sasa amethibitishwa na Umoja wa mataifa kama balozi kijana katika malengo endelevu.

Ukweli wa haraka Nchi, Majina mengine ...
Remove ads

Harakati

Alianza safari ya harakati akiwa bado yuko shule ya sekondari, kwa kujitolea katika taasisi isiyo ya kiserikali iitwayo Railegh Tanzania na Fema Klabu kama mwenye kiti wa klabu hiyo na baadae alikuwa mwanachama wa Fema National Youth Advisory Board (YAB). Katika harakati za uenezi wa masuala ya Afya ya uzazi na haki amekuwa akisaidia katika majukumu ya Fema amesaidia katika kutengeza jarida la Fema la mwaka 2016.

Amekuwa akifanya harakati katika uelekezi wa mambo ya afya ya Uzazi na haki na masuala ya kijinsia, kwa miaka mitatu sasa amekuwa akifanya kazi ya kujitolea katika UNFPA’s Youth Advisory Panel (YAP) na Afri-Yan kama katibu na Afisa Miradi , ni mtetezi mdogo wa mambo ya ya Afya ya uzazi na haki pia mambo ya masula ya kijinsia katika Femina 2017 Nguvu Ya Binti kwenye kipindi ki nachorushwa kwenye televisheni.

Jennifer Kayombo anaamini kwamba kumwezeshe mwanamke katika Nyanja za fursa na rasimali kutamsaidia kumpatia nguvu chanya katika kuubadili ulimwengu.

Remove ads

Mikutano

Katika umri wake huohuo mdogo, Jennifer amehudhuria mafunzo, warsha na mikutano mikubwa inayohusu mambo ya afya ya uzazi na haki katika nyanja za kimataifa, na amekuwa akipanga na kusaidia mipango ya ratiba mbalimbali na shughuli ambazo zilikuwa kama anzilishi katika kutoa uelekezi wa mambo ya elimu ya afya ya uzazi na haki ndani ya Tanzania.

Mwezi wa Septemba,2018 alipata nafasi yakuchaguliwa kama mmojawapo wa vijana watakuwepo kwenye jumuiya ya kukutana ya vijana,2018 ili kupata sauti za vijana wakichangia mada na kusikika katika ukumbi ujulikanao kwa jina la ukumbi wa nguvu wa huko mjini Brussels.Vijana wengine waliopata nafasi kama hiyo walitoka nchi za Pakistani,Nepal,Ethiopia,Uganda na Kenya.[1]

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads