Afya

From Wikipedia, the free encyclopedia

Afya
Remove ads

Afya ni hali ya kujisikia vizuri kimwili, kiakili, kiroho na kiutu bila kusumbuliwa na ugonjwa wowote.

Thumb
Stempu ya posta ya New Zealand, mnamo mwaka 1933.
Thumb
Mwanamke akinawa mikono 1655 hivi.
Thumb
Donald Henderson na wenzake katika kukinga watu dhidi ya ndui mwaka 1966.

Afya ya binadamu itakuwa njema kama atafuatilia kanuni na taratibu bora za afya. Hiyo inajumuisha mlo kamili, yaani chakula chenye virutubishi vyote, vikiwemo protini, wanga na mafuta (hiyo iwe katika asilimia ndogo sana).

Pia anatakiwa awe msafi mwilini na mazingira yake, kama vile kwa kuoga na kusafisha mazingira yanayomzunguka. Mandhari yenye hewa safi pia husaidia katika kuhifadhi afya ya binadamu katika mwili na akili.

Mazingira mara nyingi huchukuliwa kuwa jambo muhimu katika hali ya afya ya binadamu. Hii inajumuisha mazingira ya asili, mazingira ya kujengwa, na mazingira ya kijamii. Pia mambo kama vile maji safi na hewa, makazi salama, huchangia afya nzuri, hasa kwa afya ya watoto wachanga na watoto.[1]

Utafiti umeonyesha kuwa ukosefu wa maeneo ya burudani husabsabisha kupungua kwa afya na ustawi.[2]


Pia anatakiwa kuwa na afya ya kiroho yaani kuishi kadiri ya mafundisho ya Mwenyezi Mungu kama vile: kupendana na wengine, kuthaminiana na kuacha dhambi: mara nyingi hizo zinadhuru afya ya mwili pia.

Remove ads

Fafanuzi za afya

Sawa na suala la ugonjwa, hakuna elezo kamili kuhusu hali ya afya.


  • Kwa watu wengi ni hali ya kutosumbuliwa na maumivu na udhaifu, pamoja na uwezo wa kutumia sehemu zote za mwili. Ni wazi ya kwamba hisia hii ni tofauti kati ya mtu na mtu.
Remove ads

Majukumu

Serikali zinatarajiwa kuandaa wataalamu wa mambo ya afya na kujenga hospitali nyingi hata vijijini kwa sababu watu wengi hupoteza maisha kwa kukosa huduma za afya: hii itasaidia kupunguza vifo.

Watu wanatakiwa kuwa na ustadi wa kufanya mazoezi kwa wingi. Hata mjamzito anapaswa kufanya mazoezi, ingawa si kazi ngumu.

Pia kula mlo bora wakati wote ili kuepukana na magonjwa yanayotokana na ukosefu wa chakula fulani (virutubishi).

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads